Genesis 5:1-6

Kutoka Adamu Hadi Nuhu

(1 Nyakati 1:1-4)

1 aHii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu.

Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
2 bAliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”

3 cAdamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi. 4Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike. 5 dAdamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.

6 eSethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
Copyright information for SwhKC